Saturday, 5 June 2021

Vidoda vya tumbo vinakusumbua na hujui nini cha kufanya basi carehelp tunakupa tiba ya tatizo la vidoda vya tumbo.

VIDODA VYA TUMBO.


Vidonda vya tumbo ni tatizo linalotokea baada ya kuta za tumbo au utumbo mdogo kuwa na vidonda, hii hutokea ni baada ya kuharibika kwa ukuta wenye ute unaozuia kemikali (tindikali)za kuyeyusha chakula unaoitwa mucus. Kemikali ambayo ni acidi (tindikali)inayozalishwa mwilini kiasili husaidia kuyeyusha chakula na kuua wadudu tumboni, kama ukuta wenye ute ukiharibiwa na kushindwa kufanya kazi basi kemikali (acid) itaathiri tumbo au utumbo na kuruhusu bakteria kuendelea kusababisha vidonda vya tumbo.

Vidonda vya tumbo vinatibika kirahisi ila vikicheleweshwa bila kutibiwa huweza kusababisha tatizo kubwa. Ni tatizo linalotesa sana na kuwanyima raha watu wengi, linahitaji umakini na pia husababisha magonjwa mengine kama kansa, amoeba (amiba), homa, kupungua uzito.

 

 AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO


Kuna aina zipatazo mbili za Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers)

       1. Vidonda vya tumbo kubwa (Gastric ulcers) – Hivi ni vidonda vya tumbo vinavyotokea ndani kwenye tumbo kubwa

       2. Vidonda vya utumbo mdogo (Duodenal ulcers) – Hivi ni vidonda ambavyo hutokea kwenye utumbo mdogo (hasa juu)

 

CHANZO AU SABABU ZA VIDONDA VYA TUMBO


 

Vidonda vya tumbo vina vyanzo tofauti ili vyote ni vile vinavyohusiana na mmeng’enyo, vyanzo hivyo ni;

1 Bakteria waitwao Helicobacter pylori (H. pylori)

2 Matumizi ya dawa za kupunguza maumivu kama asprin, (NSAIDs), (Advil, Aleve, na zingine)

3 Kuwa na mawazo mengi

4 Kula vyakula vinavyozalisha acid kwa wingi

5 Kunywa pombe na vinywaji vikali

6 Uvutaji wa sigara

7 Kuto kula mlo kwa mpangilio

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO


 

Dalili za vidonda vya tumbo hujitokeza baada ya kula au kabla ya kula, ila mara nyingi wengi huwa wanazipuuzia na endelea kukuza tatizo, vidonda vya tumbo vinadalili kama;


1 Kupata maumivu ya tumbo yanayokuwa kama ya moto (kuunguza) baada na kabla ya kula

2 Kupatwa na kiungulia karibu na chembe ya moyo

3 Tumbo kujaa gesi na kuvimbiwa

4 Kichefuchefu na kutapika tena yawezekana kutapika damu

5 Kupata haja kubwa ya rangi kahawia au nyeusi yenye harufu mbaya sana, pia haja yaweza kuchanganyikana na damu

6 Kupoteza hamu ya kula na kupungua uzito

7 Kushindwa kupumua vizuri

TIBA.

 

JINSI YA KUEPUKANA NA VIDONDA VYA TUMBO

 

1 Kunywa maji mengi

2 Punguza mawazo, fanya mazoezi yatakupunguza na mawazo

3 Punguza (balansi) kiwango cha halemu (choresterol)

4 Usivute sigara

5 Punguza au acha kunywa pombe

6 Kula vizuri vyakula bora hasa asilia na sio vyakula vyenye kemikali

7 Lala vizuri kwa muda mzuri – masaa 7 hadi 9

      8    Majani ya fenugreek -chemsha kiasi cha mjani weka na chumvi kidogo kunywa mara mbili kila siku.

      9   Ndizi mbili .Ndizi zinakitu kinaitwa antibacterial substance ambao husaidia kutokua kwa vidoda tumboni kwahiyo kula ndizi moja kila siku baada ya kunywa chai asubuhi.

      10  kabichi mbichi.Tegeneza juisi ya kabichi ni nzuri sana katika kutibu vidoda  fanya kunywa juisi ya kabichi kila siku kabla ya mda wa kulala.

       11  Vitunguu.tafuna kitunguu kimoja au viwili kila siku.

       12  Nazi . Tumia maji ya nazi kunywa kadiri utavyoweza ikiwezekana kila siku itakusaidia kutibu vidoda.


No comments:

Post a Comment